Usikose Hizi Hapa

MAFUNZO YA VITENDO YAWA FURAHA KWA WANAFUNZI VYUONI

Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha,wakiwa katika mafunzo ya vitendo wakiwa darasani.

Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wametakiwa kujifunza masomo yao kwa vitendo ili kuongeza maarifa zaidi na kuleta ushindani katika soko la ajira pindi watakapoajiriwa.

Hayo yamesemwa na mkufunzi wa chuo hicho Bw;Steven Mulaki alipokuwa akihojiwa na SPIRITMWAMBA mapema leo mchana alipokuwa akiwafundisha wanafunzi wa darasa la Mt Ordizungwa.

Bw Mulaki ameongeza kwa kusema kuwa mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa vyuoni ni muhimu kwa kuwa watakapohitimu masomo yao itawasaidia kupata uzoefu watakapoajiriwa na taasisi au makampuni mbalimbali

Kwa upande wa wanafunzi wamefurahishwa na mafunzo hayo ambapo wengi wao wamemsifu mkufunzi huyo kwa kufundisha vizuri.



No comments