Usikose Hizi Hapa

Arsene Wenger, hatima yake kujulikana leo


Kocha wa Arsenal, Arsenal Wenger akishangilia Ubingwa kwa kuinua juu kombe la FA,   na mmliki wa klabu hiyo  mwenye suti nyeusi (kulia) Stan Kroenke akimpongeza

Kocha wa Arsenal, Mzee  Arsene Wenger, amefanya mkutano muhimu na mmliki wa klabu hiyo Stan Kroenke  siku ya jana  ambapo mustakabali wa mfaransa huyo ulitarajiwa kujadiliwa.

Matokeo ya mkutano huo bado hayajawekwa wazi, lakini maamuzi yanabaki baina ya Wenger na Kroenke na yatategemea pia kikao cha bodi kitakachojadili suala hilo leo hii.
Kocha wa Arsenal, Arsenal Wenger akipeana na mikono na mmliki wa klabu hiyo Stan Kroenke
Mpaka sasa bado haijajulikana kama  Mzee Wenger ataongeza mkataba ama laa baada ya kudumu katika klabu hiyo kwa miaka 21.
Masharti ya mkataba mpya yalikubaliwa miezi kadhaa iliyopita, lakini hakuna kilichofanyiwa kazi mpaka hivi sasa.
Mipango ya Mzee huyo ilikuwa  kuendelea kubaki  katika klabu hiyo lakini hali  ilibadilika  katika kipindi cha hivi karibuni  baada ya kupingwa vikali na  baadhi ya mashabiki wakihitaji  kocha huyo kuachia ngazi.
Mashabiki wa klabu ya Arsenal wakibeba mabango yanayo onyesha kumpinga kocha Arsenal Wenger
Hali kidogo imekua shwari baada ya kuifunga Chelsea  2-1  katika fainali za kombe la  FA  siku ya Jumamosi na kumfanya  Wenger  kuwa  kocha  mwenye  mafanikio zaidi  kwenye kombe hilo huku Arsenal nayo ikiwa na mafanikio zaidi kuchukua kombe hilo.

No comments