Usikose Hizi Hapa

Mancity yaicharaza Liverpool 5-0

Manchester City ime uraruwa ulinzi hafifu wa Liverpool na kunyakua ushindi mkubwa dhidi ya wageni wake wa kikosi cha wachezaji 10 Liverpool, na kufanikiwa kukwea kwenye orodha ya ligi.
Sergio Aguero alifungua mvua ya mikwaju kwa kumchenga kipa wa Liverpool Simon Mignolet.
Sadio Mane alitolewa uwanjani baada ya kunyanyua mguu wake uliomgonga kipa wa City, Ederson, aliyetibiwa uwanjani kwa dakika 10.
Gabriel Jesus aliongeza jingine na Leroy Sane kumalizia kwa mawili ya mwisho na kukamilisha ushindi wa 5-0.
Gabriel Jesus aliifunga Liverpool mabao mawili uwanjani Etihad
Kevin de Bruyne alitoa pasi safi kwa goli la ufunguzi la Aguero na pia alimtambua na kumpa pasi Jesus aliyekuwa wazi na kufanikiwa kuifungia City katika muda wa ziada baada ya kujeruhiwa kwa Ederson.
Ushindi huu unakiinusha kikosi cha Pep Guardiola juu ya mahasimu Manchester United kwenye ligi, wanaokuwa wageni wa Stoke baadaye Jumamosi.
Na unahakikisha kushindwa kwa mara ya kwanza katika msimu kwa kikosi cha Jurgen Klopp.

No comments