Usikose Hizi Hapa

KIDATO CHA NNE KESHO KUANZA MITIHANI YA MWISHO YA TAIFA...KATIBU MKUU NECTA AWAASA KUTOJIHUSISHA NA UDANGANYIFU

Watahiniwa 385,938 wanatarajiwa kutafanya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne nchini.
Akizungumza leo Jumapili, Oktoba 29,2017 Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde amesema kati ya watahiniwa hao, 323,513 ni wa shule na 62,425 ni wa kujitegemea.

Dk Msonde amesema mtihani huo utaanza kesho Oktoba 30,2017 hadi Novemba 17,2017.

Dk Msonde amesema maandalizi ya mitihani yameshakamilika."Hivi ninavyozungumza mitihani imeshafika kwenye vituo.”

Amezitaka kamati za mitihani za mikoa na halmashauri kuhakikisha utaratibu wa uendeshaji wa mitihani unafuatwa.

Katibu mtendaji huyo amewataka wanafunzi kuacha vitendo vya udanganyifu wakati wa kufanya mitihani kwa kuwa wanaweza kufaulu bila kufanya hivyo.

"Mliyojifunza yanatosha fanyeni mitihani kwa kufuata utaratibu uliowekwa," amesema.

Dk Msonde amesema baraza hilo halitasita kuwafutia mitihani wote watakaojihusisha na udanganyifu.

No comments