Usikose Hizi Hapa

SERIKALI YA YAPATA MKOPO KWA AJILI YA UJENZI WA BARABARA

Serikali ya Tanzania imepata mkopo wa Shilingi Bilioni 630.25 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika-AFDB na Mfuko wa Maendeleo ya Afrika-ADF kwa ajili ya mradi wa barabara unaoitwa TSSP yenye urefu wa Kilometa 402.979.



Mradi huo unahusisha ujenzi wa kiwango cha Lami wa barabara za Tabora-Koga-Mpanda yenye urefu wa Kilomita  335 na barabara ya Mbinga-Mbamba Bay yenye urefu wa Kilomita 67 ambapo Serikali itachangia Shilingi Bilioni 72.72.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini-TANROADS,PATRICK MHEGALE katika hafla ya utiaji saini wa mikataba minne,kati ya TANROADS na wakandarasi wanne walioshinda zabuni ya ujenzi wa mradi huo.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa MAKAME MBARAWA ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo,amesema mradi huo ni wa kihistoria kwani  tangu TANROADS ianzishwe hakujawahi kusainiwa mkataba barabara wenye urefu wa kilomita 402.

Hata hivyo Profesa MBARAWA amewaonya wakandarasi hao kutofanya udanganyifu wowote na kuwataka waharakishe ujenzi wa miradi hiyo ndani ya miezi 36 .





No comments