Usikose Hizi Hapa

MAKUMBUSHO YA TAIFA YAANDAA ONESHO LA CHIMBUKO LA BINADAMU AFRIKA

Makumbusho ya taifa la Tanzania iliyopo jijini Dar es salaam imeandaa mafunzo ya onesho la chimbuko la binadamu Afrika yanayotarajiwa kutolewa kesho.


Mkurugenzi wa Makumbusho ya taifa Prof. Audax Mabula  mafunzo na onesho hilo yanatokana na tafiti mbalimbali zinazofanyika bonde la hifadhi ya Olduvai na Laetol katika mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Aidha Prof. Audax  ameeleza onesho hilo litafanyika kesho jijini Dar es salaam na litafunguliwa na waziri wa Mali asili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na litahudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Katika onesho hilo wananchi pia wataweza kuona mambo mbalimbali ya kale ambayo binadamu wa kwanza aliweza kuyafanya katika nyanja tofauti katika maisha yake.

No comments