Usikose Hizi Hapa

SERIKALI YAPANGA KUWANUFAISHA WAJASIAMALI WADOGO KUTAFUTA SOKO LA NJE

Serikali imedhamiria kuwasaidia wajasiriamali  wadogo wadogo  kutafuta soko la nje kwa ajili ya kufikia uchumi wa kati wa viwanda nchini.


Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa  Viwanda,Uchumi na biashara Mhe,Charles Mwijage katika maadhimisho ya miaka 25 ya Tanzania  Growth Trust [TGT]   ambayo awali ilijulikana kama  Tanzania Gatsby Trust.

Mwijage amesema tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa miongoni mwa changamoto zinazowakabili wajasiriamali na wakulima wadogo wadogo ni mitaji midogo ,teknolojia duni,elimu,masoko n.k huku akifurahishwa kusikia TGT inaelekeza nguvu zake zote katika kuhakikisha inawasaidia walengwa kutatua matatizo hayo kwa kupitia programu mbalimbali kama zilivyoainishwa katika risala.

"nimetaarifiwa kwamba katika miaka 25 TGT imefanya mambo mengi sana katika sekta za ujasiriamali,kilimo,fedha (mikopo na uhamasishaji uanzishaji wa benki za wananchi) elimu ya ufundi na elimu ya juu,sayansi na teknolojia"

Aidha ameongeza kuwa serikali inatambua mchango wa TGT katika kuanzisha kitengo cha kuendeleza viwanda vya nguo na pia ameipongeza bodi ya wadhamini na wafanyakazi wa TGT,ambao wanajitolea kwa hali na mali huku bila msaada wowote kutoka serikali wameweza kufanya kazi nzuri nchini ambayo matunda yake yanaonekana dhahiri katika Tanzania Bara na Visiwani.

Kwaupande wake mtendaji mkuu wa Tanzania Growth Trust ,Oliver Lwena, ameeleza lengo la taasisi  hiyo ni kuinua  wajasiria mali na wakulima wadogo wadogo waweze  kuongeza kipato chao na kuzalisha kwa ufanisi ili kuweza kufikia   uchumi wa kati wa viwanda .

Taasisi hiyo imekua ikitoa mafunzo kwa vyuo vya kati na vyuo vikuu kufanya kazi  za kijasiriamali  pia taasisi hiyo imetoa wito kwa vijana walioko mitaani kuacha kubweteka na kutumia fursa mbali mbali zinazotolewa    ili kufikia uchumi wa kati wa viwanda.





No comments